Web Shop
   :: Reuben Kigame
   :: Mamajusi Choir
   :: Fiona Mukasa
   :: Virtue That Counts
 
   Testimonies
   :: Charles Guzo
   :: E. Tuwagiramana
   :: R. Chauganga
   :: Leah Jacob
   :: Mama Domitila
   :: Apostle Bwalya
   :: Victoria Nehale
   :: Nyisaki Chaula
 
     Resources
   :: Crossword Puzzle
   :: Amefufuka Live Radio
   :: Music Video
   :: Audio Messages
   :: Discussions
   :: Gospel Tracts
   :: About Islam
 
     Musicians
   :: Celebrate Africa
   :: Ency Mwalukasa
   :: Kirya
   :: Letwin Berebende
   :: Mamajusi Kwaya
   :: Njeri
   :: Trinity Singers
 
     Resources

Your IP:
 
 
   :: Write to us
 
Jesus



Historia Fupi ya Kwaya ya Mamajusi Moshi

Mamajusi KwayaKwaya hii ilianzishwa mnamo mwaka 1975 tarehe 11.10.1975, siku ya Jumapili saa 10:00 chini ya uongozi wa Mchungaji Kiongozi Majengo Moshi Rev. Godwin Katoto. Ilikuwa na jumla ya wanakwaya 18 wanawake na wanaume; na ikaitwa kwaya ya Uinjilisti ya Kianglikana Majengo Moshi.

Mnamo mwaka 1979 kwaya ilikwenda kurekodi kwa mara ya kwanza kule Radio Habari Maalum, Maragu - Moshi kabla ya studio kuhamishwa Arusha.

Mnamo mwaka 1980, kwaya hii ilikwenda Mvumi, Dodoma kwenye tamasha la uimbaji wa Dayosisi wakati huo ikiwa chini ya Diocese of Central Tanganyika (DODOMA D.C.T.). Pia walirekodi tena mara ya pili kwenye studio ya msalato, Dodoma mwaka huo. Vipindi vyote hivyo kwaya ilikuwa chini ya mwimbaji mwanzilishi ndugu Joseph Semaghembe ambaye pamoja na kuanzisha kwaya, bado yu mwimbaji hadi leo.

Mnamo mwaka 1982 na 1983, kwaya hii iliingia Studio ya Sauti ya Injili Moshi, na kurekodi matoleo mawili; ikiwa chini ya jina jipya: MAMAJISU KWAYA MAJENGO - MOSHI. Jina hili jipya lilizaliwa mwaka 1982 na maana ya jina hili ni - Wafalme (Mamajusi) wa Mashariki waliyoongozwa na nyota kutoka Mashariki kwenda kumwona mtoto aliyezaliwa; Mkombozo Yesu Kristo (Mathayo 2:1-6).

Pamoja na kwaya kurekodi matoleo yaliyotajwa hapo juu, manne hayakuweza kusambazwa au kutolewa kibiashara ili kujitangaza kiinjili kwa njia ya nyimbo. Matoleo ambayo kwaya inamiliki ni haya yafuatayo:

1 Ee Mungu Unirehemu 1997
2 Jee Huu Ni Wakati 1998
3 Bwana Ni Wa Ajabu 1999
4 Hey Haleluya 2000
5 Homa Ya Dunia 2001

Pia kwaya inatoleo la kwanza linalomilikiwa na Radio Habari Maalum, Arusha linaloitwa MUNGU KAUMBA.

Kwaya hii kwa sasa ina jumla ya wanakwaya sitini tu (60) na kwa sasa inamilikiwa na wakristo wa Kanisa la Kianglikana Majengo Moshi chini ya Dayosisi mpya ya mlima Kilimanjaro (Arusha DMK).